"Jamani majirani naomba
mnisaidie ananinua hukuuuuu !!!!!!! Sauti ya mwanamke akilia akiomba msaada
ikamstua Genes aliyekuwa mezani akinyoosha nguo kwa ajili ya kuwahi ibada ya
pili inayoanza saa nne za asubuhi.
Akaizima pasi na kutulia kwa sekunde kadhaa ili asikie ni wapi ilikokuwa ikitoka sauti ile.Kwa mbali akasikia kama sauti za watu wakizozana.Akapunguza sauti ya redio ili aweze kusikia vizuri sauti zile zilitokea wapi.Aliamini sauti zile za kuzozana zilitoka katika moja ya chumba cha wapangaji wenzake lakini hakuwa na uhakika ni chumba kipi.Sauti ya mwanamke akilia ikasikika tena na safari hii akaamua kuzima kabisa redio yake ili asikie vizuri.
Akaizima pasi na kutulia kwa sekunde kadhaa ili asikie ni wapi ilikokuwa ikitoka sauti ile.Kwa mbali akasikia kama sauti za watu wakizozana.Akapunguza sauti ya redio ili aweze kusikia vizuri sauti zile zilitokea wapi.Aliamini sauti zile za kuzozana zilitoka katika moja ya chumba cha wapangaji wenzake lakini hakuwa na uhakika ni chumba kipi.Sauti ya mwanamke akilia ikasikika tena na safari hii akaamua kuzima kabisa redio yake ili asikie vizuri.
"Jamani
nisaidieni ananiuaaa..!!!!!! sauti ile ya mwanamke ikarudia tena kuomba msaada
.Genes akaitambua sauti ile ,ilikuwa ni ya msichana jirani yake aitwaye Naomi
anayefanya kazi katika hoteli ya kitalii ya Mbuni lodge..
"Nini
kimetokea leo? Naomi na mumewe wanapigana ? Mbona siku zote wamekuwa wakiishi
kwa amani ? akawaza Genes na kufungua mlango wa chumba chake akatazama kama
kuna mtu yeyote pale uani ambaye alikuwa akiufuatilia ugomvi ule lakini
hakukuwa na mtu yeyote yule ambaye alionyesha kujali watu wale waliokuwa
wakipigana.Milango yote ya vyumba vya wapangaji wengine ilikuwa imefungwa na
ilionyesha walikuwa wametoka .
Naomi
na mumewe Sheddy walikuwa wakiishi chumba cha jirani na Genes.Wakati
akijishauri afanye nini mara akasikia kishindo
kikubwa katika ukuta uliounganisha chumba cha Naomi na chumba chake.
"Watauana
hawa.Ngoja nikawaamue" akawaza Genes ,na taratibu akatoka chumbani kwake
na kuelekea katika chumba cha Naomi.Akajaribu kugonga mlango kwa nguvu na kisha
akaisikia sauti ya Naomi toka ndani.
"Ingieni
mlango haujafungwa"
Genes akakinyonga kitasa na kuingia
ndani.Ghafla akajikuta amefunga breki za ghafla kwa kitu alichokishuhudia.
Naomi na mumewe Sheddy walikuwa wakipigana wakiwa wamevaa nguo za ndani
pekee.Naomi alikuwa amevaa chupi ndogo nyeupe na sidiria nyeupe iliyoyafunika matiti yake
madogo na kuyafanya yasimame na kutamanisha.Kwa sekunde kadhaa Genes alibaki
amesimama amepigwa na bumbuwazi na macho yake yalikuwa yameelekea katika mwili
ule mwororo,mweupe wa Naomi. Kwa jinsi alivyokuwa akiheshimiana na Naomi Genes
akaingiwa na woga na kutaka kurudi nje
"Genes
nisaidie anataka kuniua huyu" Naomi akaomba msaada.Genes akasitisha
kitendo alichotaka kukifanya cha kurudi nje.Badala ya kuwaamua akabaki
amemkodolea macho Naomi .
"Genes
nakuheshimu sana nakuomba tafadhali utoke ndani mwangu haraka .Usijaribu
kuingilia mambo yasiyokuhusu." Sheddy mume wa Naomi akasema kwa ukali na
kumstua Genes ambaye alikuwa ameyaelekeza macho yake kwa Naomi akiusaili mwili
ule wenye kutamanisha..
"Genes
usimsikilize huyu shetani...nisaidie ananiumiza !!! Naomi akapiga ukelele.
"Sheddy
tafadhal..............." Genes akajaribu kutamka kitu lakini Sheddy
akamzuia
"Genes
nakwambia toka humu ndani mwangu haraka sana.Nani kakupa ruhusa ya kuingia humu
ndani? Ugomvi wangu mimi na mke wangu unakuhusu nini? tafadhali ondoka haraka
sana kabla sijakufanyia kitu kibaya " Sheddy akasema kwa ukali huku
ameikamata mikono ya Naomi kwa nguvu
"Genes
nisaidie ananiumizaa!!!!! .....Naomi akalia huku akijitahidi kujitoa katika
mikono ya Sheddy.Genes akamuonea huruma Naomi alivyokuwa akilia akashikwa na
hasira
"
Sheddy nakuomba tafadhali usiendelee kumpiga mkeo.Nakuomba ndugu yangu niko
chini ya miguu yako muache mkeo.Unamuumiza " Genes akasema taratibu
akijaribu kumsihi Sheddy amuachie mkewe.
"Genes
naona hujanifahamu vizuri mimi ni nani.Nimekwambia ugomvi wangu mimi na mke
wangu unakuhusu kitu gani? Tafadhali ondoka humu ndani mwangu haraka."
Sheddy akafoka.
"Mshenzi
wewe humu ni kwako? Una kitu chochote unachoweza kusema ni chako humu ? "
Naomi akamwambia Sheddy kwa ukali.Kwa hasira Sheddy akamnasa kibao kizito.
"Malaya
mkubwa wewe..nimekwisha kuonya siku nyingi juu ya matusi yako unayonitukana.Umepata
kiburi baada ya mwanaume wako kuja kukusaidia? Ngoja sasa niwaonyeshe adabu
wewe na malaya mwenzako" Sheddy akasema kwa ukali.Kauli ile na kitendo cha
kumnasa Naomi kibao vikamkasirisha sana Genes.Kwa nguvu akamvaa Sheddy na
kumsukuma akaangukia kitandani.Naomi akaitumia nafasi hiyo kuchukua kitenge na
kujifunga kisha akatoka nje huku akilia
"Inuka
sasa upigane na mimi wewe si kidume?Nakwambia inuka upigane na mwanaume
mwenzako" Genes akasema akiwa amefura kwa hasira.
"Genes
nimekwambia toka ndani mwangu haraka sana.Nitakuitia mwizi sasa hivi!!! akasema
Sheddy kwa ukali akiwa amekaa kitandani
"Nimekwambia
inuka unipige mimi badala ya mkeo...." akasema tena Genes kwa kujiamini
"Genes
nimekwambia toka ndani mwangu.Unaingilia mambo yasiyokuhusu kwa nini? Ugomvi
kati yangu mimi na mke wangu unakuhusu nini?Halafu huna hata adabu unaingia
ndani mwangu bila hodi na kutukuta tukiwa watupu" akafoka Sheddy
"Hata
kama ni mkeo,hupaswi kumpiga kama mnyama.Nimekufahamu muda mrefu sana lakini
sikutegemea kama unaweza ukafanya kitendo cha aibu kama hiki cha kumpiga mkeo
bila huruma.Umenishangaza sana Sheddy.Kwa taarifa yako ni kwamba siku hizi wanawake hawapigwi kama
unavyofanya.Wanawake wameamka na wanadai haki zao.Akikupeleka katika vyombo
vinavyohusika na haki za wanawake unaweza ukachukuliwa hatua kali sana."
Genes akasema na kuanza kuipunguza jazba aliyokuwa nayo.
"Genes
wewe huna mke na huelewi matatizo tunayokumbana nayo sisi watu tunaoishi na
wanawake ndani.Siku ukioa ndiyo utafahamu haya ninayokwambia.Huyu Naomi
unayemtetea amebadilika sana siku hizi.Amekuwa na kiburi cha ajabu .Sijui ni
kwa nini amebadlika namna hii.Ninahisi kuna mwanume amempata ambaye anampa
kiburi.Naomi hakuwa hivi.Naomi hakuwa mtu anayesimama na kujibizana na
mimi" Sheddy akasema
"hata
kama amekukosea Sheddy hukupaswa kumpiga.Kama mwanaume ulitakiwa uwe na busara
ukae chini na mkeo na muongee kama mke na mume na kisha muyamalize matatizo
yenu na maisha yaendelee.Ninamfahamu Naomi vizuri na sidhani kama ana tabia
kama hizo unazohisi anazo.Mbona mkeo ni mtu anayejiheshimu sana tofauti na
wanawake wengine hapa mtaani.Jaribu kukaa na mkeo muongee na muyarekebishe yale
yote yaliyotokea.Mnapopigana mnajiabisha ninyi wenyewe.Mnawafaidisha majirani
ambao wanabaki wanawacheka kila mpitapo.Tafadhali ndugu yangu nakuomba kama
mwanaume mwenzangu kaa na mkeo na mjaribu kutafuta suluhu ya matatizo
yenu." Genes akasema na mara mlango ukafunguliwa Naomi akaingia akiwa
ameongozana na balozi wa mtaa mzee Msuya pamoja na wazee wengine wawili.
"Kijana nini kimetokea? Mbona
mwenzio amekuja ameniletea malalamiko kwamba umekuwa ukimpiga ? Balozi mzee
Msuya akamuuliza Sheddy ambaye akamtazama na kisha kwa dharau akauliza
"wewe
unaongea kama nani? Mambo yangu mimi na mke wangu yanakuhusu nini?
Mzee Msuya akaangaliana na wale wazee wenzake
kisha akamgeukia Sheddy na kusema
"Sikiliza
kijana.Mimi ni balozi wa mtaa huu .Ninamfahamu Naomi toka alipohamia hapa mtaani.Ni
mwanamke anayejiheshimu sana na sikutegema kama siku moja ungeweza kumfanyia kitendo
kama hiki cha kumpiga.Nimekuja hapa kusikiliza sababu iliyopelekea wewe kumpiga
mkeo na kumuumiza mkono namna hii kabla sijamruhusu aende mbele zaidi kwa hatua
stahiki dhidi yako."
"Balozi
mimi nakushangaa sana mtu mzima kama wewe kuanza kuingilia ugomzi wa vijana
.Naomba jamani muondoke humu ndani na mniache mimi na mke wangu tuyamalize
mambo yetu sisi wenyewe.Naomba mkaendelee na kazi zenu" Akasema Sheddy.
“Kijana
naomba uwe na adabu kwa wazee wako.Usiongee kama vile unaongea na wahuni
wenzako huko mitaani.Nina uwezo wa kukuchukulia hatua sasa hivi" akafoka
mzee Msuya
"Unichukulie
hatua kwa kosa lipi wewe mzee? Ugomvi haukuhusu wewe unaingilia Mimi
nimekwaruzana na mke wangu wewe yanakuhusu nini?..." Akasema Sheddy kwa
ukali .
"Kijana
nakuomba uwe na adabu tafadhali.Msikilize balozi wako anataka kusema nini"
akasema mzee mmoja kati ya wale wawili waliokuwa wameongozana na balozi Msuya
"Balozi
mimi sitaki malumbano zaidi na huyu mtu.Ninachokisema ni kwamba nimechoka naye
na simuhitaji tena hapa kwangu.Ninachotaka yeye achukue begi lake na aondoke
zake sitaki tena kumuona hapa ndani kwangu." Naomi akasema kwa ukali akiwa
amesimama nyuma ya balozi.
"
Kijana umesikia mwenzako anavyosema ? Amekuchoka na hataki tena kukuona ndani
kwake." Akasema balozi Msuya
"Hapa
si kwake.Hapa ni kwangu mimi na hana nguvu yoyote ya kunitoa humu.Kama ni kuondoka aondoke yeye" akasema Sheddy
.Mzee Msuya aamwangalia kwa makini na kusema
"Kwanza
mimi sikufahamu kabisa katika orodha ya watu wangu wa mtaa huu. Ninayemfahamu
ni Naomi pekee.Wewe si mtu wa mtaa huu.Nakuomba kijana usiendelee kufanya fujo
hapa.Nitaita askari sasa hivi waje wakuchukue na kukuweka ndani." akasema
balozi Msuya.
'Niwekwe
ndani kwa kosa lipi? Kugombana na mke wangu nikawekwe ndani? akauliza Sheddy
kwa ukali
"Huyu
kijana anaonekana hanifahamu vizuri" Mzee Msuya akasema na kuchukua simu
yake akazitafuta namba fulani na kupiga.
"Halo
Afande Sadiki.Habari yako ndugu yangu" akasema mzee Msuya
"Afande
ninaomba msaada wako wa haraka.Kuna kijana mmoja amevamia chumba cha msichana
mmoja hapa mtaani kwangu na analeta fujo,amempiga na hataki kutoka .Naomba
unitumie vijana wawili ili waweze kutusaidia kumtoa kijana huyu" akasema
mzee Msuya akatulia kusikiliza upande wa pili wa simu na kisha akasema
"Nashukuru
sana afande.Waelekeze wafike pale nyumbani kwangu " akamaliza kuongea na simu na kuikata kisha
akamgeukia Sheddy
"
Nilikuwa naongea na mkuu wa kituo .Anawatuma askari wawili sasa hivi ili
wakuchukue wakakuweke ndani " akasema mzee Msuya.
"Lakini
huu ni uonevu jamani.Kwa nini lakini mnafanya namna hii? Kwa nini mnavunja ndoa
yangu? akalalamika Sheddy.Naomi aaonyesha kukerwa na kauli ile ya Sheddy
"Ndoa
! Umemuoa nani hapa? Nimesema chukua begi lako na uondoke sitaki kukuona
tena ndani kwangu." Akasema Naomi
huku akilichukua begi dogo la kijani na kuanza kupakia nguo za Sheddy.Sheddy
ambaye alikuwa amekaa kitandani akiwa amevaa nguo ya ndani pekee akainuka na
kuvaa suruali yake na shati halafu
akavaa viatu vyake vya kuchomeka.
"Begi
lako hili hapa.Naomba uondoke na sitaki tena kukuona hapa kwangu" Naomi
akasema akiliweka begi mezani.
"Kweli
Naomi unadiriki kunifukuza? Sheddy akamuuliza Naomi huku akimuangalia kwa jicho
kali.
"Sheddy
jaribu kuwa mwelewa.Mwenzako amekwisha kuambia kwamba ondoka nyumbani kwake na
ndiyo sababu ya kuita uongozi wa mtaa kama
mashahidi.Unapoendela kumghasi ghasi kwa maswali unafikiri atabadili
mawazo yake? Chukua mizgo yako na uondoke umuache mwenzio aishi mwenyewe kwa
amani" Genes akasema
"
Tulia wewe mtoto wa kiume mwenye kimbele
mbele kama mwnamke.Mambo hayakuhusu unayaingilia kama nini sijui" akafoka
Sheddy.Kauli ile ikamkasirisha sana Genes akaliinua begi dogo la Sheddy
akalirusha nje na kisha akaanza kumsukuma Sheddy kutoka mle ndani.
"Wewe
mwanaume gani unayeishi kama ndege? Huna makao maalum.Kumbe kiburi chote hiki
hata shuka la kujifunika huna? Ondoka
ndani mwa watu muache mtoto wa watu apumzike.Amechoka kukulea baba mzima
kama wewe" Akasema kwa kejeli Genes.Sheddy akarusha ngumi kwa dhumuni la
kutaka kumpiga Genes usoni lakini Genes akawahi kuidaka.
"Sitaki
kupigana na wewe Sheddy.Sitaki kuharibu siku yangu bure.Nakuomba uondoke kwa
amani kabla polisi hawajafika hapa" akasema Genes
"
Nakwambia hivi ,tutaonana mtaani..Lazima nikutafute nkuonyeshe kwamba sisi ndio
wenye mji huu.Nitakufanyia kitu kibaya sana.na wewe Naomi ninakuambia
utanitambua mimi ni nani.lazima nikuonyeshe kazi malaya mkubwa wewe."
akatamba Sheddy
"Kijana
tafadhali usiendelee kutukana watu hapa.Umekwisha pewa mizigo yako ondoka kwa
amani.Naomi hakuna kitu kingine amekisahau huyu kijana ili kesho asirudi tena
hapa? akauliza mzee Msuya
"Hapana
mzee Msuya.Kila kitu chake nimemuwekea humo katika begi lake."akajibu
Naomi
"
haya kijana safari njema" Mzee Msuya akasema.Sheddy akageuka na kumtazama
kwa macho makali
"na
wewe mzee lazima nikushikishe adabu.We si ndiyo kinara wa kuvunja nyumba za
watu basi nitakuonyesha kwamba mimi ndo mtoto wa mjni haswaa....subiri mziki wangu
unakuja" akasema Sheddy huku akiliinua begi lake na kulivaa mgongoni
akaanza kupiga hatua kuondoka huku akitukana.
"Haya
mama sasa uko salama .Jitahidi huyu kijana asije akarudi tena hapa.Hafai kabisa
.Kijana ana dharau sana”
akasema mzee Msuya
"Samahani
sana mzee Msuya kwa dharau alizozionyesha kwako.Yule ndivyo alivyo ana dharau
nyingi sana." Akasema Naomi kwa adabu.
"Usijali
Naomi .Ila ninakuonya kama mwanangu tulia na utapata mwanaume mwenye tabia
njema,mwanaume anayekujali na mwenye heshima kwako,kwa kila mtu na
anayejiheshimu yeye mwenyewe,si kama huyu kijana sijui ulimtoa wapi."
"Nashukuru
sana mzee Msuya kwa kunisaidia kumuondoa huyu kijana hapa kwangu endapo
ningekuwa mimi peke nisingeweza kumtoa hapa kwa sababu alikwisha kataa kutoka kabisa.Kwa
mambo niliyoyapata wakati nikiwa na kijana huyu sintafanya makosa tena ya
kurukia rukia wanaume wasiokuwa na mbele wala nyuma.Nimejifunza mengi na safari
hii nitakuwa makini sana na hawa vijana wasiokuwa na mwelekeo " akasema
Naomi
"Mimi
nakushauri pia uende polisi ukatoe maelezo ili wawe na kumbu kumbu kwa sababu
wote tumesikia akikutishia maisha yako.Iwapo utapatwa na jambo lolote lile basi
tutajua ni yeye ndiye anayehusika." Genes akasema
"
Hilo ni wazo zuri sana umelitoa.Yule kijana anaweza kweli akamdhuru mwenzake.Si
mwema kabisa yule kijana.Usipuuze alichokisema nenda polisi ukatoe maelezo na
watakuwa na kumbu kumbu ili kama kuna jambo lolote baya litakutokea basi tujue
ni yeye ndiye mhusika mkuu." Akashauri mzee Msuya
"Nashukuru
sana Genes kwa kunisaidia.Samahani sana kwa kukupotezea wakati wako"
akasema Naomi
"Usijali
Naomi ,iwapo akirudi tena na kuanza kukuletea fujo usisite kuniambia ili
nimpeleke mimi mwenyewe polisi.Mjinga yule amesababaisha hadi nimechelewa
ibada" akasema Genes
"ouh
samahani sana Genes." akasema Naomi
"Usijali
Naomi.Nitasali hata ibada ya kwenye Televisheni" akasema Genes na
kuwafanya watu wote waangue kicheko.
"Msicheke.Ni
kweli nitasali ibada ile itakayo onyeshwa katika luninga." Genes
akasema huku akielekea ndani
mwake.Akajitupa kitandani na kuanza kukumbuka kila kitu kilichokuwa
kimetokea.Picha ya Naomi akiwa amevaa nguo ya ndani ndogo nyeupe pamoja na
sidiria nyeupe iliyoyafanya matiti yake madogo kusimama ilimjia usoji na
kumfanya akishike kichwa chake kwa mikono yake miwili.
"Sikutegema
kama siku moja ningekuja kumuona Naomi akiwa katika hali ile.Naomi ni mwanamke
mrembo na anayejiheshimu sana .Toka amehamia katika nyumba hii nimekuwa
nikitafuta nafasi ya kujaribu kuwa naye karibu lakini nimeshindwa.Leo kama
bahati nafanikiwa kumuona akiwa mtupu namna ile.Nilipomuona mwiloi mzima
ukanisisimka .Lazima nikiri kwamba Naomi ni msichana mzuri.Namsifu mwenyezi
Mungu kwa uumbaji wake uliotukuka kwani pale alitulia na akatuumbia pambo la
dunia.Sijui kwa nini mtoto kama yule hajashiriki mashindano ya urembo.Nina
imani angeweza kushika nafasi za juu sana kama angeshiriki kwa sababu ana
vigezo vyote vya kumuwezesha kuwa mrembo maarufu..Sjui yule muhuni alimpa nini
Naomi hadi akashawishika kuishi naye.Kweli mapenzi ni sawa na upofu kwa sababu
Naomi hakuwa saizi ya yule mlevi Sheddy.Naomi anatakiwa awe na mwanaume mwenye
kujua nini thamani ya mwanamke.Mwanaume mwenye kujua kupenda." akawaza
Genes kisha akainuka pale kitandani na kukumbuka kwamba alikuwa amezima redio
wakati akienda kuamua ugomvi.akaiwasha redio yake akaketi sofani na kuendelea kuwaza.
"Sura
ya Naomi bado inanijia akilini kila sekunde.Siwezi kuacha kumuwaza mtoto mzuri
kama Naomi.Nadhani hii ni nafasi ambayo natakiwa kuitumia ili kuwa karibu na Naomi.Lazima
niitumie nafasi hii kikamilifu ili niweze kumpata msichana yule mwenye uzuri wa
kipekee kabisa.Nitaanza kwanza kwa kujenga mazoea naye ya ukaribu na hasa
katika kipindi hiki ambacho ameachana na jamaa yake anahitaji kuwa na mtu wa
kuweza kumliwaza na kumfanya asahau yale yote yaliyopita.Hii ni nafasi yangu
.Sitakiwi kufanya makosa .Lazima nifanye kila aina ya jitihada ili niweze
kumpata Naomi.Siku nyingi nimekuwa
nikimuwaza lakini nilimuheshimu kwa kuwa alikuwa akiishi na bwana wake.Kwa sasa
yuko huru na sitaki tena kuipoteza nafasi hii adimu." akawaza Genes.Akawasha pasi na kuendelea kunyoosha
nguo zake.Kazi ya kunyoosha nguo ilikuwa ngumu sana kwani kila mara sura ya
Naomi ikawa inamjia kichwani na kumfanya aache kunyoosha na kukaa akiwaza.
* * * *
Sauti
ya mlango kugongwa ndiyo iliyomstua Genes toka usingizini.Alikuwa amelala toka
saa kumi za jioni.Taratibu akainuka na kwenda kuufungua mlango.Mlangoni alikuwa
amesimama msichana mwenye uzuri wa shani Naomi akiwa na tabasamu lenye
aibu kwa mbali.Genes akapatwa na mstuko
kidogo kwa jinsi Naomi alivyokuwa amependeza.Alikuwa akiushangaa uzuri wa Naomi
jioni hii .Kwa namna alivyokuwa akimuangalia ni kana kwamba ilikuwa ni mara ya
kwanza kumuona.Naomi pia aligundua kwamba Genes alikuwa akimuangalia akaona
aibu na kutazama chini.
"Naomi
karibu sana" akasema Genes baada ya Naomi kuanza kuangalia chini
alipogundua kwamba Genes alikuwa akimuangalia
"Genes
samahani kwa kukusumbua.Sikujua kama ulikuwa umelala" akasema Naomi.
"Usijali
Naomi.Nilikuwa nimejipumzisha si unajua tena inatubidi kujiandaa kwa ajili ya
kesho kazini" akasema Genes huku akitabasamu
"
Karibu ndani Naomi" akasema Genes na kuufungua mlango zaidi ili Naomi
apite.Jioni hii Naomi alikuwa amependeza vilivyo ndani ya mavazi meupe.Huku
akiona aibu Naomi akaingia chumbani kwa Genes.Mkononi alikuwa ameshika mfuko
mweusi wa nailoni.
"Karibu
kiti Naomi" Genes akamkaribisha Naomi kiti.
"Ahsante
sana Genes" akajibu Naomi na kuketi sofani.Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa
Naomi kuingia chumbani kwa Genes.
"Naomi
unatumia kinywaji gani? akauliza genes akiwa ameushika mlango wa friji.
"Nashukuru
sana Genes ,naomba usisumbuke kwani nimetoka kunywa soda muda si mrefu"
akajibu Naomi
"Ni
mara ya kwanza kuingia kwangu nakuomba uniachie walau baraka kidogo kwa kunywa
walau glasi moja ya soda." Genes akasisitiza.Naomi kwa aibu akakubali
"
Habari za Jumapili? Genes akaanzisha maongezi baada ya kumpatia Naomi kinywaji
"Habari
nzuri Genes.Sijui wewe umeshindaje?
"Mimi
nimeshinda salama.Kutwa nzima ya leo nilikuwa nimepumzika ndani" akasema
Genes kisha akapiga funda moja la kinywaji kilichokuwa katika glasi yake.
"Genes
nimekuja kukushukuru kwa msaada wako ulionisaidia wa kuweza kumtoa yule jamaa
ndani kwangu.Nilikwisha jaribu kutaka kumuondoa lakini nikashindwa kwa sababu
kila nilipojaribu kumwambia simuhitaji tena alinitishia kuniua ikanibidi kukaa
kimya.Vile vile samahani sana kwa matusi yote aliyokuwa amekutukana."
Naomi akasema huku akiangalia chini .Uso wa Genes ukajenga tabasamu pana sana.
"Usijali
Naomi.Ni mambo ya kawaida kutokea na wala wewe si wa kwanza kukorofishana na
mumeo." Akasema Genes na kumfanya Naomi atabasamu akainua kichwa na kusema
"Yule
hakuwa mume .Ni mtu niliamua kuishi naye lakini hatukuwa na mipango yoyote ya
mbeleni kwamba tuoane na kuwa mke na mume" Naomi akasema
"
Sikufurahishwa na kitendo alichokifanya cha kukupiga ndiyo maana nilipandwa na
hasira nikataka kupigana naye." Genes akasema huku akicheka kichini chini
"Du
! pole sana Genes.Ulifanya kazi kubwa sana ya kumuondoa yule jamaa kwangu.Bila
ya wewe sijui ingekuwaje leo.Nahisi pengine angeniulia ndani" Naomi
akasema
"Kwa
sasa jitahidi kutokuwa na mawasiliano naye ya namna yoyote ile .Jitahidi kuishi
mwenyewe na kuyatengeneza maisha yako.NI wakati wako wa kujijenga" akasema
Genes
"Kweli
kabisa Genes.Natakiwa niitumia nafasi hii kujitenegenezea msingi mzuri wa
maisha" akasema Naomi na kuimalizia soda iliyokuwamo katika glasi lake
"Genes
mimi si mkaaji sana .Nina kazi za kufanya usiku huu ambazo kesho natakiwa
niziwahishe kazini.Kuna mzigo huu kidogo nimekuletea." Akasema Naomi huku
akiinuka pale sofani.
"Nashukuru
sana Naomi.Siku yoyote muda wowote ukihitaji msaada wa namna yoyote usisite
kuniambia.Au kama akirudi yule jamaa na kuanza kukuletea fujo usiogope
kunitaarifu.Nitamkamata na kumpeleka polisi mimi mwenyewe.Si katika shida
tu,hata siku ukijisikia mpweke na unahitaji mtu wa kuongea naye na
kubadilishana mawazo mimi niko hapa,usisite kunigongea mlango au hata kunipigia
simu.Naomba unipatie namba yako ya simu kwani sikuwa na namba yako katika simu
yangu.Si vibaya mara moja " Genes akasema na kisha wakabadilishana namba
na Naomi akaondoka.
Baada
ya Naomi kuondoka Genes akaufunga mlango na kusimama kwa sekunde kadhaa akiwa
amekishika kiuno chake na uso wake umejengeka kwa tabasamu pana sana.Akaiendea
soda aliyokuwa amebakiza Naomi katika chupa akaibusu na kuinywa.
"Nahisi
ni kama vile niko ndotoni.Naomi leo ameingia chumbani kwangu !! .Hii ni dalili
njema sana.Huu ni mwanzo mzuri sana" akawaza Genes.
"Humu
kwenye huu mfuko kuna nini? akasema taratibu Genes huku akiufungua mfuko ule na
kukuta kuna nyama ya kuku ya kukaanga.
"Wow
! ...Naomi... I love you so much.Nakupenda sana Naomi..Laiti ungejua ni namna
gani moyo wangu unakuhitaji ungenionea huruma" Genes akasema taratibu
akakibusu kigaja cha mkono wake na kukipuliza kuelekea chumba cha Naomi.
ENDELEA KUFUATILIA MFULULIZO WA SIMULIZI HII KILA SIKU HAPA MASIMULIZI
Huu ni lazima ushuhudia usomaji na kila mtu, nipo hapa kuruhusu ulimwengu wote kujua kuhusu mtu aliyeokoa uhusiano wangu na mtu huyu mkuu anaitwa Dr IZOYA. Hakika alifanya kazi nzuri kwangu kwa kumrudisha mpenzi wangu wa zamani ambaye aliniacha na kuahidi kamwe kurudi kwangu tena. Kwa hili, nimekuja kutambua kuwa kutoa maelezo ya Dk IZOYA kwa ulimwengu utafanya mengi mazuri kwa wale walio na nyumba zilizovunja au uhusiano kwa ajili yake ili kukusaidia kurekebisha uhusiano huo uliovunjika au ndoa yako. Unaweza kumfikia kupitia anwani yake ya barua pepe: drizayaomosolution@gmail.com au kumwita moja kwa moja kwenye [+12098373537]. Kuwasiliana naye na kuona jinsi tatizo lako litatatuliwa ndani ya 24hours. Pia mtaalamu katika mambo yafuatayo ...
ReplyDelete(1) Unataka kurudi nyuma yako.
(2) Unataka kukuzwa katika ofisi yako.
(3) Unataka wanaume / wanawake kukufuate.
(4) Unataka mtoto.
(5) Wewe ni mjasiriamali na unataka kushinda mikataba
(6) Unataka mume wako awe wako milele
(7) Unahitaji msaada wa kiroho.
(8) Umeshambuliwa na unataka kupona fedha zilizopotea.
(9) Weka talaka
(10) Kualika kwa mila ya fedha
(11) Chagua uchaguzi