MASIMULIZI
Saturday, April 26, 2014
BLEEDING HEART SEHEMU YA 22
RIWAYA : BLEEDING HEART
SEHEMU YA 22
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Joe are you still there?
“I’m here my love’ akajibu Joe huku akijifuta jasho.
“Niambie Joe ,ndoto hii inaweza kuwa ni kweli? Ni kweli siku moja utaondoka na kuniacha peke yangu? “ akauliza Swazi huku akilia na kumfanya Joe akae kimya
“Nijibu Joe..mbona umekaa kimya..? akaendelea kusisitiza Swazi.Joe akavuta pumzi ndefu na kusema
“swazi naomba tuonane tafadhali.Kuna jambo la muhimu sana la kujadili “
“Jambo gani Joe mbona unaanza kuniogopesha? Akasema Swazi
“Kuna jambo la dharura limejitokeza ambalo inatubidi kulijadili “
Swazi akavuta pumzi ndefu na kuuliza
“Tukutane wapi?
“Naomba uje Manzini..ni muhimu sana” akasisitiza Joe
“Ok nakuja sasa hivi.Umenipa wasi wasi sana Joe”
“Usiogope malaika wangu.Niko hapa nyumbani kwangu ninakusubiri” akasema Joe na kukata simu.
“Inaniuma sana kumuacha Swazi peke yake,lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kwenda kumuuguza mama yangu.Swazi ataumia mno akisikia kuhusu jambo hili kwa sababu tayari mimi ni sehemu ya maisha yake..” akawaza Joe akielekea chumbani kwake
ENDELEA………………………………..
“Joe hapana ,huwezi kuondoka ukaniacha hapa peke yangu.Sahau kuhusu kuondoka” swazi akasema kwa sauti kali huku akilia baada ya Joe kumuoyesha barua ya uhamisho wa kuhamia jijini Dar es salaam.Alikuwa amekaa chini akilia .Joe akamuonea huruma akamfuata pale chini akamuinua na kumuweka kitandani
“Swazi nafahamu ni namna gani nilivyo mtu muhimu kwako.Naomba vile vile ufahamu kwamba wewe ni mtu muhimu sana katika maisha yangu.Sikutegema kama suala hili lingetokea katika kipindi hiki kifupi tulichokaa pamoja.Ninakupenda sana na siku zote wewe utaendelea kuwa moyoni mwangu.Utaendelea kuishi moyoni mwangu”
“Nothing you can tell me can make me change my decision..I’ve said you are not going and its final” akasema Swazi huku akizidi kulia akiwa amemkumbatia Joe.
Joe akampiga piga mgongoni na mara swazi akainua kichwa.
“Joe do you real love me?
“ Yes I do” akajibu Joe
“Look into my eyez and tell me that you love me and you wont leave me alone in this hell” akasema Swazi akimtazama Joe Usoni.
“swazi naomba unisikilize.Uhamisho huu si kwamba ni mimi ndiye nimeomba.Ofisi yetu imeamua kunihamisha baada ya maombi ya baba yangu kuomba niwe karibu na familia yangu katika kipindi hiki ambacho mama yangu anaumwa.Its abaout my mother swazi..My own mother..kwa sababu yake inanibidi nikubaliane na uhamisho huu.Tafadhali swazi naomba tusiyafanye mambo haya yakawa magumu kwa sababu hakuna kitu ninachoweza kukibadilisha kwa sasa.Ninahitaji kuwa na familia yangu kwa wakati huu.Swazi naomba ufahamu kwamba wewe ni mtu muhimu sana katika maisha yangu na siku zote utakuwa hapa moyoni mwangu na nitakupenda milele.Nitakuwa nikija mara kwa mara kuja kukuona na kukaa nawe” akasema Joe na kumfanya swazi azidi kulia
“Samhani Joe kwa kuwa mbinafsi na kusahau kuhusu ugonjwa wa mama yako.Hii imetokana na kulewa na penzi lako kiasi kwamba siwezi kukaa mbali nawe kwa hofu ya kuibiwa na wanawake wengine.Kama ulivyosema kwamba maamuzi yamekwisha fanywa na hatuwezi kuyapangua.Japokuwa roho inaniuma sana lakini sina namna ya kuweza kukuzuia usiondoke na kurudi nyumbani kwenda kumuuguza mama yako.Kama ingekuwa ni kwa uwezo wangu nisingekubali kamwe uondoke na kuniacha hapa peke yangu.Sina mtu mwingine wa karibu hapa Swaziland na katika dunai nzima ambaye anaweza akanipa furaha kama ninayokuwa nayo nikiwa nawe.Wewe ni malaika wangu na siku zote utaendelea kuwa wangu.Sintakuacha kamwe na sintakubali hata siku moja mwanamke mwingine akuchukue toka mikononi mwangu.Joe penzi lako limenifanya nisione mwanaume mwingine zaidi yako na kwa maana hiyo niko tayari kwenda hadi mwisho wa dunia kwa dhumuni moja tu la kuwa nawe.Nitafanya kila niawezalo kwa ajili ya kuwa nawe tena.Nitakuja Tanzania muda si mrefu kwa dhumuni moja tu la kuwa nawe karibu.Nitakutafuta usiku na mchana mpaka nikupate.Ila naomba nikukumbushe kwamba wewe ni wangu peke yangu na sintakubali hata siku moja kukuona ukiwa na mwanamke mwingine ambaye si mimi.Sikutishi ila nitaumia mno na kutokana na maumivu hayo nitakayoyapata ninaweza kufanya jambo lolote.Naomba ujichunge sana Joe na usijaribu kuwa na mwanamke mwingine.Niko tayari kuja kukuona kila mwisho wa wiki kwa sababu uwezo huo ninao .Sitaki kuwe na umbali kati yangu nawe.Nakupenda sana Joe zaidi ya unavyoweza kufikiri” Swazi akasema kwa hisia kali na kukilaza kichwa chake kifuani kwa Joe ambaye alimshukuru Mungu kwa Swazi kukubali japo kwa shingo upande yeye kurudi nyumbani.Wakiwa katika hali ya simanzi kubwa mara kunasikika muungurumo wa gari nje ya nyumba yao.Joe akainuka na kwenda kuchungulia dirishani.Nguvu zikamuisha baada ya kuwaona polisi watatu wakishuka ndani ya gari wakiwa wameongozana na mtu mmoja mnene aliyekuwa amevaa mavaziya kiutamaduni ya watu wa Swaziland.Joe akatetemeka na kijasho chembamba kumtoka.Haraka haraka akamuita Swazi.
“Polisi wamekuja.Tutafanya nini? Akauliza Joe kwa wasi wasi Swazi akasogea dirishani kuchungulia naye akajikuta akiufumba mdomo wake kwa mshangao.
“Ni Ndlamane Dlamini…msaidizi wa mfalme..”
“What ! akauliza Joe kwa mshangao
“ Ni msaidizi wa mfalme ..lazima wamegundua kwamba niko humu..wamekuwa wakinifuatilia kwa muda mrefu sana nyendo zangu…”
“sasa tutafanya nini? Akauliza Joe
“Usiwe na wasi wasi..let me handle this..” akasema Swazi na mara kengele ya mlango ikalia.Joe mwili ulikuwa ukimtetemeka kwa hofu.Hakujua afanye nini kwa wakati huo.Alihisi kama vile miguu imefungwa na haina nguvu tena.
Joe alikuwa akitetemeka mwili mzima baada ya mlango kugongwa.Hakujua afanye nini au awaepuke vipi wale maaskari waliokuwa pale nje ya nyumba yake.Kwa mara ya kwanza alijilaumu sana kwa kuwa na mahusianao na Swazi huku akifahamu fika kwamba Swazi ni mke wa mfalme
"Ee mungu nisaidie katika suala hili ambalo tayari limekuwa gumu kwa upande wangu" Joe akaomba kimoyo moyo huku akihema kwa nguvu.Alikuwa amechanganyikiwa na hakujua angefanya nini.Swazi akamtazama kwa makini usoni na kuliona jasho likimchuruzika.Akamsogelea na kumkumbatia bila ya wasi wasi wowote.
"Usiwe na wasi wasi wowote Joe.Nimekwambia niachie mimi suala hili nitalimaliza.Naomba uniamini.Tafadhali tulia na wala usiwe na wasi wasi wowote." Swazi akambusu na kujaribu kumpooza moyo Joe ambaye midomo ilikuwa ikimtetemeka kwa woga.
Mlango uliendelea kugongwa kwa nguvu,Taratibu Swazi akauendea na kuufungua.Akakutanisha macho na
Ndlamane Dlamini
msaidizi mkuu wa mfalme.
Ndlamane
alimuangalia Swazi kwa macho makali sana na kumwambia.
" Swazi hamsini zako zimetimia.Mambo ambayo umekuwa ukiyafanya na kijana huyu yote tunayafahamu na leo ndiyo ,mwisho wenu" akasema kwa ukali
Ndlamane
.
"
Ndlamane
wewe ni msaidizi tu wa mfalme na huna nafasi yoyote ile ya kuweza kuyafuatilia maisha yangu na wala huna maamuzi yoyote kuhusiana na maisha yangu.Nakuomba uondoke na uniache mimi niishi maisha yangu nitakavyo.Si wewe wala huyo mkuu wako anayeweza kunipangia namna ya kuishi maisha yangu.Tafadhali naomba uondoke humu ndani haraka sana" akasema Swazi kwa ukali akiwa amesimama mlangoni.
"Swazi wewe ni mke wa mfalme wa ukoo wetu na hilo unalifahamu fika.Kwa nini unaamua kumsaliti mfalme na kuwa na mahusiano na huyu kijana? Hilo ni kosa kubwa umelifanya.Umevunja taratibu zetu na kwa hilo unastahili adhabu kali sana." akasema
Ndlamane Dlamini
kwa ukali huku akimtazama Swazi kwa macho makali .
"Nimekwisha kuambia kwamba si wewe au huyo bosi wako unayemuita mfalme mnaweza mkanipangia maisha yangu.Kwa miaka mingi nimevumilia kila aina ya taabu na mateso mliyonipatia wewe na huyo mfalme wako .Ninasema kwamba imetosha na sintovumilia tena aina yoyote ile ya mateso.Niko tayari kwa lolote mtakalotaka kulifanya na sioni sababu yoyote ya kuendelea kuziheshimu mila hizi kandamizi ambazo zimenifanya miaka hii yote niishi maisha magumu ya taabu na mateso makali .Mila hizi hazitambui thamani yangu mimi kama binadamu mwenye haki kama binadmau wengine.Ninawatuma mpeleke taarifa kwa hao viongozi wenu waliowatuma kwamba mimi siogopi kitu chochote na niko tayari kwa jambo lolote lile" Swazi akasema kwa ukali
Ndlamane
akamtazama Swazi usoni kwa sekunde kadhaa na kusema
" Sitaki kuongea sana Swazi kwa sababu suala lako liko mikononi mwa baraza la wazee ndio watakaokuhukumu kwa mujibu wa mila na taratibu.Nimekuja hapa si kwa ajili ya kulumbana nawe bali kutekeleza maagizo ya viongozi wangu ." akasema
Ndlamane
"Mmetumwa kuja kunichunguza ninafanya nini siyo? akauliza Swazi kwa ukali zaidi
"Nasema hivi,nendeni mkawaambie hao viongozi wenu kwamba mmemkuta Swazi akiwa na mpenzi wake wakifanya mapenzi.Niko na mpenzi wangu,malaika wangu tofauti na huyo mfalme wenu ambaye mnamuabudu na kumtukuza kama Mungu wenu.Naomba mumpelekee ujumbe kwamba siku yoyote akijaribu tena kutia mguu nyumbani kwangu na kunifanyia kitendo kama mlichonifanyia wakati ule nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe." akasema Swazi na kuuma meno kuonyesha hasira alizokuwa nazo kisha akauhsika mlango na kutaka kuufunga lakini mikono yenye nguvu ya
Ndlamane
ikauzuia .
"Swazi huna haja ya kukasirika kwa sababu hatujaja hapa kwa shari.Kilichotuleta hapa tumekuja kumchukua huyo kijana uliye naye ndani" A akasema taratibu na kumfanya Swazi astuke
"Mtaka kumchukua Joe? Nani kawatuma na mnataka kumpeleka wapi? akauliza Swazi kwa mshangao
"Tumetumwa na wakuu wetu tumchukue Joe.Wapi anakwenda na anatakiwa kwa makosa gani nadhani wewe ndiye mwenye majibu yote" akasema
Ndlamane
"Hapana Joe hatoki humu ndani.Hata angewatuma nani ,nawaambia kwamba Joe humu ndani hatoki na hamumpeleki kokote kule." Swazi akasema kwa ukali akiwa ameuzuia mlango
Joe akiwa ndani alikuwa ameloa jasho.Swazi na
Ndlamane
walikuwa wakiongea lugha ya Siswati ambayo Joe hakuwa akiilewa sawa sawa lakini alikuwa akifahamu baadhi ya maneno na aliweza kugundua kwamba ni yeye ndiye alyekuwa akiongelewa pale mlangoni na hii akamzidishia hofu.Laiti kama kungekuwa na mlango mwingine wa kuweza kutoka na kukimbia basi angeweza kukimbia na kutokomea mbali kabisa.Aliamini kwamba huko anakotaka kupelekwa hakukuwa kuzuri kabisa kwake.Alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wa mfalme.Hakujua adhabu yake ni nini lakini alichokuwa akikifahamu ni kwamba jambo hili linaweza kumsababishia adabu kali ya kifungo cha muda mrefu gerezani.Kila alipowaza kuhusu kwenda kukaa gerezani kwa kipindi kirefu alizidi kuchanganyikiwa kwa sababu alikuwa akitakiwa nyumbani Tanzanzia haraka iwezekanavyo kwa ajili ya kuwa karibu na mama yake ambaye alikuwa akisumbuliwa na saratani.
"Nimesema Joe haendi kokote kule.Nendeni mkapeleke ujumbe huo kwa hao waliowatuma kwamba nimesema Joe hatoki humu na haendi mahala kokote kule." Swazi akasema kwa sauti kubwa
Ndlamane
akamtazama swazi na kisha kwa sura iliyoonyesha kwamba hakuwa na masihara hata kidogo akasema
"Swazi tafadhali naomba upishe njia ili tufanye kazi iliyotuleta.Usijaribu kuyafanya mambo yakawa magumu zaidi" akaamuru
Ndlamane
" Fanyeni lolote lile ambalo mnaweza lakini humu ndani Joe hatoki" Swazi akasema tena kwa ukali
Ndlamane
akawageukia askari na kuwapa ishara kwamba waingie ndani kwa nguvu na kumchukua Joe.Purukushani ikatokea pale mlangoni ,askari wakitaka kuingia ndani na swazi akiwazuia kuingia.Kwa kutumia nguvu wakamuangusha Swazi chini na kuingia ndani.
"jamani naomba kuwe na amani.hakuna haja ya kuwa na vurugu." Joe akasema baada ya kuwaona askari wamesimama pale sebuleni wakimuelekezea bunduki na Swazi akiwa amelala chini akilia
"Tafadhalini naomba mnieleze kuna tatizo gani? Joe kauliza
"wewe ndiwe Joe?
Ndlamane
akauliza
"Ndiye mimi.Kuna tatizo gani? Joe akauliza
"Ninaitwa
Ndlamane dlamini
.ni msaidizi mkuu wa mfalme...............Joe tafadhali naomba uongozane nasi .Tuna shida na wewe.Unahitajika kwa ajili ya mahojiano muhimu sana"
Ndlamane
akamwambia Joe.
"Nimefanya kosa gani?" Joe akauliza
"hata sisi hatuelewi ila tumetumwa na viongozi wetu tuje tukuchukue.Tafadhali ongozana nasi"
Ndlamane
akaamuru.
"Sijakataa kuongozana nanyi kwenda mahala kokote lakini naomba mtambue kwamba mimi si raia wa nchi hii na kuna sheria za kimataifa ambazo zinanilinda kwa maana hiyo naomba kwanza niwasiliane na mwanasheria ili suala hili liweze kwenda kisheria zaidi" Joe akasema kwa ujasiri mkubwa.Ile hali ya uoga aliokuwa nayo mwanzo ilikwisha anza kumtoka.Swazi alikuwa amelala chini akiendelea kulia
"tafadhali Joe nakuomba unisikilize ninachokuambia .Nimepewa ruhusa ya kutumia nguvu kama ikinilazimu kufanya hivyo na ndiyo maana unaniona niko hapa na hawa maaskari.Nakuomba Joe kubali kuongozana nasi bila vurugu yoyote.Hakuna haja ya mwanasheria kwa sababu hupelekwi mahakamani kwa hiyo usiwe na hofu na jambo lolote lile." akasema
Ndlamane
kwa sauti ya taratibu.
"Joe usikubali kuongozana nao...Hawa ni.........." swazi akasema lakini kabla hajamaliza Joe akamkatisha
"Swazi hakuna haja ya kulumbana na hawa jamaa,niache niongozane nao kwenda huko wanakotaka niende.Usijali nitakuwa salama" Joe akasema huku akipiga hatua kuelekea nje.Swazi naye akainuka.
"Kama mnamchukua Joe ,basi tuchukueni sote wawili.Tuhukumuni sote
wawili"
Swazi akasema kwa ukali huku akilia.
"Swazi tafadhali,nakuheshimu sana na sipendi kuona nguvu inatumika ili kukutuliza.Joe ameamua kuongozana nasi kwa hiari yake mwenyewe nakuomba usijarbu kuyafanya mambo haya kuwa magumu zaidi.Naomba utuache tufanye kazi yetu"
Ndlamane
akasema
"Swazi tafadhali naomba usiwe na wasi wasi.Nitakuwa salama." Joe akajaribu tena kumtoa wasi wasi Swazi huku akiingia katika gari la polisi.
" Ninakufuata Joe.Nataka kufahamu kinachoendelea " Swazi akasema.huku naye akiingia katika gari lake
taratibu gari la polisi likaondoka huku Swazi akilifuata kwa nyuma kutaka kujua nini kitatokea kwa Joe.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO…………………..
0 comments:
Post a Comment
Followers
MAHABA
SERENA
BEFORE I DIE
I DIED TO SAVE PRESIDENT
FAIDIKA NA MASIMULIZI
DEATH MESSENGER
CHOMBEZO ZA MASIMULIZI
MISS TANZANIA PART 2
Blog Archieves
April 2014
(57)
About Me
pettysean.blogspot.com
View my complete profile
Total Pageviews
726,876
BONYEZA "LIKE" NA UJIUNGE NASI MOJA KWA MOJA KWA SIMULIZI MPYA KILA SIKU
Powered By
masimulizi
0 comments:
Post a Comment