MASIMULIZI
Wednesday, April 9, 2014
TEN CHAPTERS SEHEMU YA 8
RIWAYA : TEN CHAPTERS
SEHEMU YA 8
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Saa tisa za usiku sherehe ikafungwa .Bado Naomi aliendelea kupongezwa na wafanyakazi wenzake kwa kuifanya sherehe ile kuwa na mvuto wa aina yake.Baada ya kuagana na watu wengine Naomi na Genes wakaingia katika gari lao na kuondoka.
" Sherehe ilipendeza sana " akasema Genes wakiwa garini lakini Naomi hakujibu kitu.Genes akakumbuka kwamba Naomi hakupenda maongezi wakati akiendesha gari.
Waliiacha barabara iliyokuwa ikielekea nyumbani kwao wakachepuka kushoto .Genes akafikiri Naomi amepotea njia lakini kila alipomtazama hakutaka kuamini kama ni kweli Naomi amepotea njia.
Baada ya mwendo wa dakika kumi hivi gari ya Naomi ikapunguza mwendo na kuwasha taa ya kushoto kuashiria kwamba ilikuwa ikielekea katika geti la hoteli kubwa ya kitalii ya Kobe Village moja ya hoteli kubwa na yenye hadhi ya juu katika ukanda huu wa afrika mashariki.Naomi akalipeleka gari hadi katika maegesho kisha akamgeukia Genes.Akauinua mkono wake wa kushoto akamshika bega Genes.Wakatazamana kisha Naomi akasema
" Genes usiku wa leo tutalala hapa.."
Genes akamtazama Naomi asiamini kile alichokisikia.
"Naomi unasemaje? Huku akitabasamu Naomi akasema
" Genes usiku wa leo tutalala hapa " akarudia Naomi halafu akafungua mlango wa gari na kushuka..Genes ambaye alionekana kama vile amemwagiwa maji ya baridi naye akashuka garini.Naomi akamshika mkono wakaanza kupiga hatua kuelekea ndani ya hoteli ile kubwa ya kifahari.
ENDELEA...................................................
Genes hakuongea kitu alibaki anamuangalia Naomi ambaye alikuwa akitembea kwa kasi kuelekea ndani ya hoteli kana kwamba hakuwa akihitaji kuonekana na mtu yeyote akiingia pale hotelini.Genes alimfuata nyuma huku akijiuliza maswali mengi kuhusiana na kitendo kile cha Naomi kuamua kulala katika hoteli ile ya kifahari bila kumfahamisha toka awali.
" Simwelewi Naomi kwa nini ameamua tulale hapa usiku wa leo.Hajanieleza sababu ya sisi kulala hapa .Hatukuwa tumepanga kulala hapa .Inaonekana amedhamiria kabisa kwamba lazima tulale hapa hotelini na hakutaka hata kunipa nafasi ya kumuuliza ni kwa nini ameamua tulale hapa hotelini badala ya kurejea majumbani kwetu.Ngoja nimkubalie kulala hapa ili nisimuharibie furaha yake aliyonayo leo.Endapo nitakataa kulala hapa ninaweza nikaipoteza furaha yote aliyonayo na hivyo kutia doa harakati zangu za kumpata malaika huyu.Sijawahi kumuona Naomi akiwa na furaha kama aliyonayo usiku wa leo.Toka nimefahamu sijawahi kumuona akiwa na furaha ya namna hii.Uso wake umejawa Nuru na tabasamu la aina yake.Nadhani nimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa usiku wa leo kumfanya naomi ajione ni wa pekee kabisa.I made her queen of the night.I lifted her to the top.Kila mtu aliyekuwepo katika shetrehe ile macho yake yalikuwa kwa Naomi.Hakutegemea kama jioni yake ya leo ingekuwa nzuri na ya kupendeza namna hii.Kwa kweli lazima nimsifie mrembo huyu kwa usiku wa leo amependeza isivyo kawaida.She's amazing.Anazidi kunivutia kila dakika ninayokuwa naye karibu kiasi cha kunifanya nitake kuwa naye kila sekunde." Akawaza Genes akiwa nyuma ya Naomi wakipanda ngazi kuelekea mapokezi.Alikuwa akimuangalia Naomi huku akitabasamu.
" She's so sexy.Ana mvuto wa kipekee kabisa na wa aina yake.Anavyotembea ni kama hataki kukanyaga ardhi.Naomi amebarikiwa uzuri wa asili .Najisikia fahari kubwa kuwa karibu naye kwa usiku wa leo na kupata heshima kubwa.Hii ilikuwa ni ndoto yangu ya siku nyingi ya kutaka kuwa karibu na msichana huyu anayeufanya moyo wangu ukose utulivu kila nimuonapo.Sielewi ni kwa nini aliamua kupoteza muda wake mwingi kwa kuwa katika mahusiano na yule kijana muhuni ambaye hakuwa saizi yake.Naomi anahitaji mwanaume ambaye atamtunza atamjali,atamthamini na kumpa furaha maishani.Mwanaume ambaye atahakikisha kwamba lile tabasamu la kimalaika alilonalo Naomi haliondoki usoni pake hadi siku anaingia kaburini.That man is me.Ninajiamini ninaweza kuyafanya hayo yote kwa sababu ninampenda sana Naomi.Nimempenda toka siku ya kwanza jicho langu lilipomuona na toka siku ile nimeendelea kumpenda Naomi kila siku.Nimekuwa nikiomba usiku na mchana niweze kuipata walau nafasi ya kuweza kuwa karibu na mrembo huyu na leo Mungu amesikia maombi yangu na tazama leo hii nina kwenda kulala hoteli moja na mtu ambaye nimekuwa nikimuotya usiku na mchana .Naona ni kama muujiza fulani hivi.Dunia hii imejaa maajabu mengi sana.Pamoja na hayo ninajipongeza hata mimi mwenyewe kwani hatua hii niliyofikia si ndogo.Ninaamini tayari nimeanza kuingia taratibu katika maisha ya Naomi na usiku wa leo nimejizolea alama za kutosha.Harakati zangu zinaendelea vizuri .Nitafanya kila niwezalo ili niweze kumpata Naomi .Siwezi kumuacha akaondoka mikononi mwangu na kutua katika mikono ya mwanaume mwingine.Mimi ndiye mwanaume wa maisha yake." Genes akakatishwa mawazo yake na sauti ya Naomi akisalimiana na wahudumu wa mapokezi.Ilionekana ni kama vile walikuwa wakifahamiana kwa sababau baada ya salamu walitaniana kidogo ikiwa ni pamoja na kumsifia Naomi namna alivyopendeza usiku huu..Baada ya maongezi ya dakika kama mbili hivi Naomi akamtambulisha Genes kwa wahudumu wale.
" Huyu hapa ni rafiki yangu anaitwa Genes" akasema Naomi akimtambulisha Genes kwa wale wahudumu wa mapokezi.Genes akatabasamu.halafu akasalimiana na wale wahudumu.Mhudumu mmoja akachukua ufunguo toka katika kabati maalum la kuhifadhia funguo akampatia Naomi.
" Kila kitu ni kama ulivyoelekeza" akasema muhudumu yule wakati akimpatia Naomi ufunguo na kumfanya Genes ajiulize maswali mengi.
" Ina maana Naomi alikwisha weka oda ya chumba tayari? Lakini mbona alifanya mambo haya kwa siri bila kunishirikisha na mimi? Halafu mbona funguo yenyewe ni moja? Ina maana mimi na yeye tutalala katika chumba kimoja? akawaza Genes kisha akatabasamu.
"Hvi ni kweli mimi na Naomi tunakwenda kulala chumba kimoja? naona ni kama muujiza mkubwa .Ni kitu ambacho sikukitarajia kama kingeweza kutokea mapema namna hii.Japokuwa siwezi kukataa kwamba moyo wangu umefurahia sana kwa mafanikio haya makubwa na ya haraka ya kuwa karibu na Naomi namna hii lakini bado nina maswali mengi kichwani kuhusiana na jambo hili." akawaza Genes na mara Naomi akamshika mkono
" Twende zetu Genes " akasema Naomi wakaanza kuondoka kuelekea chumbani.Genes alijitahidi kutabasamu ili kumridhisha Naomi .
" My first night with Naomi..mhh ! " akawaza Genes .Walikuwa wakitembea kimya kimya kueleka chumbani.
"Tonight its just me and you Genes..Siwezi kusubiri zaidi ya hapa..Uvumilivu umenishinda .Siwezi kuendelea kuutesa moyo wangu wakati uwezo wa kukwambia ukweli ninao.Vyovyote vile atakavyonichukulia I dont care..Nina kila sababu za kuamini kwamba genes ndiye mwanaume wa maisha yangu.Ana kila kitu ninachikihitaji toka kwa mwanaume wa ndoto zangu.Siwezi kuendelea kupoteza muda wakati mwanaume ninaye mikononi mwangu.Siwezi kusubiri anitamkie yeye ..Nataka asubuhi ya kesho niamke nikiwa mikononi mwa Genes.Sina hakika na hisia zake kwangu lakini ninakila sababu ya kuamini kwamba hata yeye ananipenda lakini anasita kunieleza ukweli wa hisia zake.Nitamuanza mimi kumweleza na wala sintaogopa kitu.Nikiendelea kusubiri wanawake wengine watamnyakua genes toka mikononi mwangu..Sitaki jambo hilo litokee na ndio maana tonight its the night of truth..Kuna msemo usemao try and fail but dont fail to try.." akawaza Naomi wakati wakitembea kimya kimya kuelekea katika chumba ambacho watalala kwa usiku huo.
Hatimaye wakafika katika chumba namba 104.Naomi akachomeka ufunguo katika kitasa na kuufungua ule mlango na kuingia ndani.
" Karibnu ndani Genes" akasema Naomi .
" Ahsante sana Naomi": akajibu Genes na kuingia mle chumbani.Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri sana.Naomi akafunga mlango na kwenda kuketi katika sofa alilokuwa ameketi Genes.Akamwangalia Genes na kutabasamu na kisha akasema.
" Genes leo nina furaha ya ajabu sana.I'm so excited..I've never felt this way before...Nashindwa nikueleze vipi ili uweze kunielewa.Furaha niliyonayo haielezeki.Ninajihisi ni kama vile ninapaa mawinguni.I'm so happy Genes ..so Happy" akasema Naomi .Genes akatabasamu na kusema.
" Naomi nimefurahi sana kukuona ukiwa na furaha ya namna hiyo.Toka nimekufahamu sijawahi hata mara moja kukuona ukiwa na furaha ya namna hii.You deserve it.You deserve happiness.Nitafurahi zaidi kama hilo tabasamu lako halitatoweka usoni mwako “ akasema Genes huku akitabasamu.
“ Genes furaha hii niliyonayo leo isingewezekana bila ya wewe.Wewe ndiye uliyenifanya leo hii nikawa na furaha ya aina
yake.Genes naomba ufahamu kwamba umenifanyia mambo makubwa sana usiku wa leo ambayo sikuyategemea kabisa .Katika usiku wa leo nimepata heshima kubwa toka kwa wafanyakazi wenzangu na yote hii ni kwa sababu ya uwepo wako pembeni yangu.Genes sioni neno zuri zaidi la kiswahili la kuonyesha shukrani zangu kwako zaidi ya ahsante sana.” akasema Naomi.Genes akatabasamu na kusema
“ Naomi kama nilivyokwambia awali kwamba unastahili kuwa na furaha hii kubwa.Ninafurahi kuwa mmoja wa watu wenye kuchangia kuleta tabasamu katika uso wako .Ninajisikia fahari kubwa kuwa karibu na mtu kama wewe ..." akasema Genes
Taratibu Naomi akainuka pale sofani na kuelekea katika friji.
" Genes unatumia kinywaji gani usiku huu? akauliza Naomi huku akilifungua friji.
" Chochote kile ambacho utapendezwa nikitumie nitafurahi sana" akasema Genes huku akiilegeza tai yake.Naomi akachukua vipande vya barafu akaweka katika glasi na kumimina mvinyo.
" Genes kwa furaha niliyonayo leo naomba tugonganishe glasi na kutakiana furaha ya kudumu maishani" akasema Naomi na kila mmoja akainua glasi yake juu.
" Kwa furaha ya kudumu maishani cheers !! " wakasema wote kwa pamoja na kugonganisha glasi zao na kila mmoja akanywa funda moja.Naomi akaweka glasi mezani akamtazama Genes kisha akatabasamu
" Genes najua unajiuliza mswali mengi sana kwa nini tuko hapa usiku wa leo.? akasema Naomi huku akimuangalia Genes ambaye hakujibu kitu zaidi ya kutabasamu.Naomi akaendelea
"Genes kwanza kabisa naomba radhi kwa kutokufahamisha toka mapema kuhusu suala la kuja hapa hotelini usiku huu.Haikuwa dhamira yangu kufanya hivi .Sikuwa nimepanga kama nitakuja hapa hotelini usiku huu .Maamuzi ya kuja hapa niliyafanya tukiwa ukumbini hivyo nikamtumia ujumbe wa simu Latifa rafiki yangu yule tuliyemkuta mapokezi, aniandalie chumba kimoja kwa ajili yangu na mgeni wangu.Kilichonifanya nifanye maamuzi hayo ni kutokana na furaha ya ajabu niliyoipata tukiwa ukumbini.Nilihisi kama niko katika dunia nyingine kabisa.Nilihisi ni kama ninaelea mawinguni.Wewe ndiye uliyenifanya nikawa na furaha kubwa na ya aina yake .Sikutaka furaha hii iishie ukumbini pekee.Nilihitaji niendelee kufurahi zaidi na zaidi nikiwa nawe.Hii ni sababu kubwa iliyonifanya niamue kuchukua chumba na kuja hapa na wewe baada ya sherehe kumalizika.Endapo tungerudi nyumbani kila mmoja angejifungia chumbani kwake na kulala na furaha yangu ingeishia hapo.Genes naomba ufahamu kitu kimoja kwamba wewe ni sababau ya furaha yangu.You made me feel like a woman..not just a woman but a respectable woman.Nimeheshimika na kuthaminiwa kwa sababu yako...Genes..." Naomi akasita kuendelea ,akamtazama Genes usoni kisha akachukua glasi yake ya mvinyo akanywa funda moja na kusema.
" Genes ,kwa muda huu mfupi ambao nimekuwa nawe kama rafiki na mtu wangu wa karibu ,naomba nikiri kwamba ninajiona ni msichana mwenye mabadiliko makubwa sana.Najiona niko tofauti sana na Naomi yule wa kipindi cha nyuma.Umenifanya nijitambue zaidi.Kwa sasa ninaiona thamani yangu na maisha yangu.Nimekuwa na mtazamo mpya wa maisha yangu ya sasa na ya baadae.Ninajiamini zaidi.Kwa ujumla Genes una mchango mkubwa katika mabadiliko haya makubwa ya maisha yangu kitu kinachokufanya uwe ni mtu wa muhimu sana kwangu.Ni sababu hiyo inayonifanya nijikute nikihitaji kuwa nawe kila dakika.Nikiwa nawe najua nitacheka , nitafurahi na kuhisi furaha ya ajabu" Naomi akanyamaza akachukua glasi yake ya mvinyo akanywa .Genes akafungua mdomo wake na kutaka kusema kitu lakini Naomi akawahi kumzuia
" Let me finish Genes" akasema Naomi ambaye kwa usiku huu alionekana kuwa mwongeaji sana hasa kutokana na mvinyo ambao amekuwa akinywa mfululizo.
" Genes nafahamu kwamba kuwa nawe kila saa kila dakika ni jambo lisilowezekana kutokana na majukumu tuliyonayo.Kwa mfano kuanzia jumatatu sintakuwepo kwa muda wa mwezi mmoja.Nitakuwa katika hoteli yetu mpya iliyofunguliwa Zanzibar.Kuna shughuli ninakwenda kuifanya kule.Kwa maana hiyo kwa muda wa mwezi mzima sintaiona sura yako.Genes nimekuzoea sana na kumaliza mwezi mzima bila kuitia machoni sura yako kwangu mimi ni kama mwaka na ndiyo maana nimeona walau kwa usiku huu mmoja tukawa pamoja ,tukafurahi pamoja.One night just for you and me.Nimekuzoea ghafla sana Genes na sitaki kuwa mbali nawe hata kidogo. Kwa maana hiyo ninataka kuutumia usiku wa leo kuwa nawe kwa sababu sintakuona kwa muda wa mwezi mzima.Tafadhali Genes naomba ukubali kwamba utakuwa nami usiku wa leo na ninaomba usikasirike kwa maamuzi haya ya kuja hapa hotelini .Nimefanya hivi kwa kuogopa pengine ningekwambia mapema ungenikatalia..Just for tonight Genes" Akasema Naomi huku akimuangalia Genes kwa huruma.Genes alikaa kimya akimtazama Naomi.
" Say yes genes " akasema Naomi kwa sauti laini ye kubembeleza baada ya kuona Genes hajibu chochote.Genes akatabasamu na kusema.
" Naomi sipati neno zuri la kuweza kuielezea furaha niliyonayo.Furaha hii kubwa niliyonayo inatokana na mambo mawili.Kwanza nina furaha kubwa kukuona ukiwa na furaha sana siku ya leo.Ninapokuona ukiwa na furaha kiasi hiki ninafarijika na kujawa na furaha mara mbili zaidi yako.Kama rafiki na mtu wako wa karibu nitajitahidi kuhakikisha kwamba furaha hii uliyonayo inadumu milele.Tabasamu hili la kimalaika lililoko usoni mwako halikauki milele" akasema Genes na kumfanya naomi acheke kicheko laini na uso wake ukachanua kwa tabasamu pana sana.
" Thank you Genes you are so sweet" akasema Naomi.Genes akatabasamu na kusema .
" sababu ya pili inayonifanya nijawe na furaha ni kuwa karibu nawe .Kwa muda mrefu nimekuwa nikitafuta nafasi ya kuwa nawe karibu kama marafiki nikaikosa kutokana na wewe kuwa tayari katika mahusiano.Namshukuru Mungu kwa sababu nimeipata tena nafasi hii ya kuwa karibu nawe.Natamani ukaribu huu uendelee milele na milele ili niweze kuufurahia ucheshi wako,kusuuzika moyo na na tabasamu lako adhimu,na kama usemi usemao ukikaa karibu na waridi na wewe utanukia harufu ya waridi,ninataka niwe karibu nawe ewe waridi ili niweze kunukia.Kuhusu kuwa nawe hapa hotelini kwa usiku huu nakosa neno zuri la kuweza kukueleza namna nilivyofurahi kwa nafasi hii adimu sana. Hukupaswa kuogopa kunitaarifu kuhusu kuja hapa hotelini.Nisingeweza kukukatalia Naomi.Jambo lolote ambalo linakupa wewe furaha niko tayari kulifanya" akasema genes ..Kikapita kimya cha dakika moja Naomi akasema
" Genes bado hujajibu swali langu nilikuuliza kwamba uko tayari kuwa nami kwa usiku huu? .Jibu ndiyo au hapana " akasema Naomi.Genes akanywa funda moja la mvinyo halafu akasema
" Naomi hakuna mwanaume yeyote katika dunia hii anayeweza kukataa ombi lako la kutaka kuwa naye hasa kwa usiku kama huu.Kulijibu swali uliloniuliza jibu ni ndiyo..ntakuwa nawe kwa usiku huu " akasema genes.Naomi akainuka kwa furaha na kwenda kumkumbatia . " Ouh Genes ,thank you..thank you so much" Akasema Naomi kwa furaha halafu akaenda kuchukua chupa ya mvinyo na kujiongezea katika glasi .
" Naomi kuna jambo nataka kukuuliza" akasema Genes kwa sautui yenye wasi wasi fulani ndani yake.
" Uliza Genes" akajibu Naomi
" Mbona umechukua chumba kimoja badala ya viwili? Tutalala vipi? Akauliza Genes huku akicheka..Naomi naye akatabasamu na kusema
" Tutalala humu humu .Chumba hiki ni kikubwa na kina nafasi ya kutosha kwa watu wawili.Dhumuni la kutaka tusirudi majumbani kwetu ni kutaka kuwa karibu nawe.I want you close to me tonight..Kwa maana hiyo tutalala chumba kimoja na kitanda kimoja.Are you scared? akasema Naomi kwa sauti laini huku mkono wake mmoja ukilisugua sugua bega la Genes.
" Genes unaogopa kulala na mimi kitanda kimoja? Akauliza tena Naomi huku akimuangalia Genes kwa macho malegevu.Genes akahisi damu inaanza kumchemka.
" Ouh my ! Hivi ni kweli au ninaota? Naomi anataka kulala nami kitanda kimoja !! Naona ni kama muujiza huu.." Akawaza Genes akiwa ameyaelekeza macho yake katika sehemu za kifua cha Naomi.Kuna kitu kilimvutia na kumfanya asiyabandue macho yake pale.Naomi naye alikuwa kimya ameyaelekeza macho yake kwa Genes.Alionekana akihema haraka haraka.
" Mbona hunijibu Genes.Unaogopa kulala na mimi kitanda kimoja?
Genes akayaondoa macho yake kifuani kwa Naomi akakohoa kidogo na kusema
" Siogopi naomi..Nimekosa neno la kusema .This is a great suprise to me" Akasema Genes halafu akameza mate.
" Usijali Genes,hakuna ubaya wala tatizo lolote kama tukilala kitanda kimoja.Tunaweza tukalala bila kufanya hivyo unavyofikiria" akasema Naomi na kumfanya Genes acheke kicheko kikubwa
" Genes I can read your mind..Ninafahamu kitu gani unawaza" akasema huku akicheka.Akachukua glasi yake na kunywa funda moja la mvinyo halafu akamgeukia Genes.
" Kicheko hicho kinamaanisha niyasemayo yana ukweli.Asilimia kubwa ya vijana wa kiume wakiwa peke yao na vijana wa kike haijalishi kama ni wapenzi au ni marafiki ,mara nyingi huwaza kitu kimoja tu,Ngono.Mawazo yao yote wanayaelekeza huko.Lakini inawezekana kabisa kwa mvulana na msichana wakakaa pamoja katika chumba kama hiki na ,wakala chakula pamoja.wakanywa,waacheka na kufurahi,wakabadilishana mawazo juu ya mambo mbali mbali ya maisha ya kila siku bila kuhusisha mawazo ya ngono" akasema Naomi na kumfanya Genes atabasamu
" Nakubaliana nawe Naomi.Unachokisema ni kitu cha kweli kabisa.Kwa upande wangu mawazo hayakuwa huko unakofikiri yalikuwa." akasema genes huku akicheka.
" Usijali Genes hayo ni mambo ya kawaida kwa wanadamu kwa sababu tumeumbwa na hisia.Wakati wote mwanaume na mwanamke wanapokutana Faragha kama tulivyo mimi na wewe sasa hivi basi hisia kama hizo lazima ziwepo hasa kama ni wapenzi au kama kuna hisia za kimapenzi kati yao.Sisi si wapenzi ,ni marafiki wa kawaida na sijui kama kuna hisia zozote za kimapenzi katika urafiki wetu." akasema Naomi kisha akaichukua glasi yake ya mvinyo na kupiga funda mbili
" Sijui nimwambie ukweli kwamba yeye ndiye chaguo langu.Kila dakika inayosonga ninajikuta nikizidi kumpenda zaidi na zaidi.Lakini ngoja nivute subira kidogo ili urafiki wetu uzidi kukomaa ndipo nimweleze ukweli .Nataka nimwonyeshe kwamba sina tamaa ya ngono na ninamuheshiu yeye na mwili wake .Nina uhakika mkubwa kwamba kitu pekee ambacho Naomi anakihitaji kwa usiku wa leo ni kufanya mapenzi.Japokuwa hajaweka wazi lakini ni suala ambalo liko wazi kabisa.Ili kuzidi kuijenga heshima baina yetu na kumfanya azidi kuvutika na mimi ,nitalala naye kitanda kimoja lakini nitajizuia kufanya naye mapenzi.Ni jambo gumu lakini sina budi kujitahidi." akawaza Genes mara akastuliwa na sauti ya Naomi
" Genes..." akaita Naomi.Genes akainua kichwa na kumtazama.
" Nahisi joto sana..Nataka nikaoge nipunguze hili joto " akasema Naomi huku akiinuka pale sofani na kuelekea kitandani.
" Naomi ngoja nikupishe ili uweze kubadili nguo na kwenda kuoga.I'll be outside" akasema Genes huku akiinuka.
" Hapana Genes huna haja ya kutoka.Unaogopa kitugani? akasema Naomi huku akitabasamu
" Siogopi kitu ila si adabu njema kukaa humu ndani wakati ukibadilisha nguo." akasema Genes.
" Usihofu kitu Genes..kwani kitu gani ambacho hujakiona ? Siku ile ulipokuja kuamua ugomvi wangu na Sheddy si ulinikuta nikiwa na nguo za ndani pekee..ukanitazama mwili wangu wote sasa leo unaogopa nini? Kuna kitu gani hukukiona siku ile? Huna haja ya kuogopa kitu Genes..just relax.." akasema Naomi kwa sauti ambayo ilionyesha wazi kwamba tayari alikwisha lewa.Genes akaketi sofani na mara Naomi akafungua zipu ya gauni lake na kuliacha lianguke chini ,akabakiwa na nguo za ndani pekee.Mwili wa Genes ukapatwa na mstuko mkubwa kama chaji za umeme zimempitia.Akabaki ameduwaa akimkodolea macho msichana yule mweupe aliyekuwa amesimama pale kitandani akiwa amebakiwa na nguo nyeupe za ndani .Naomi akainama na kuliokota gauni lake akaliweka kitandani.Kitendo kile kikayafanya maungo nyeti ya Genes kupoteza utulivu.
" Ouh My Gosh ! .." akasema Genes kwa sauti ndogo ambayo Naomi hakuweza kuisikia
" Tonight you must be mine Genes..Its just you and me..Asubuhi ya kesho nitaamka nikiwa mikononi mwako..Sina muda wa kusubiri zaidi ya hapa.I cant wait any longer. " akawaza Naomi huku akijifunga taulo .
NINI KITATOKEA HUMO CHUMBANI ? MPENZI MSOMAJI TUKUTANE TENA KATIKA SEHEMU IJAYO
KWA SIMULIZI ZAIDI TEMBELEA HAPA MASIMULIZI KILA SIKU
0 comments:
Post a Comment
Followers
MAHABA
SERENA
BEFORE I DIE
I DIED TO SAVE PRESIDENT
FAIDIKA NA MASIMULIZI
DEATH MESSENGER
CHOMBEZO ZA MASIMULIZI
MISS TANZANIA PART 2
Blog Archieves
April 2014
(57)
About Me
pettysean.blogspot.com
View my complete profile
Total Pageviews
BONYEZA "LIKE" NA UJIUNGE NASI MOJA KWA MOJA KWA SIMULIZI MPYA KILA SIKU
Powered By
masimulizi
0 comments:
Post a Comment