Tuesday, April 15, 2014

BEFORE I DIE SEHEMU YA 13






            “Latoya ,labda kwa kukupa picha halisi ya msichana huyu ni kwamba Marina ni binti mdogo ambaye nilimkuta akifanya biashara ya ukahaba katika moja ya kumbi  za burudani.Nilipomuona nilijikuta nikiguswa sana ,kwanza kwa umri wake na pili kwa ile biashara aliyokuwa akiifanya.Nilifanya jitihada za kuonana naye nikijifanya ni mteja ninayehitaji huduma ya ngono .Tulipokuwa hotelini nilimweleza kuhusu lengo langu la kutaka kumsaidia ili aweze kuondokana na maisha yale yasioendana na umri wake.Alinieleza historia yake.Ni mtoto asiyekuwa na wazazi wala ndugu yeyote hapa mjini.Ndugu yake pekee anayemfahamu alikuwa ni mama yake ambaye alifariki miaka kadhaa iliyopita hivyo kumfanya Marina kujiingiza katika biashara hii ya kuuza mwili ili aweze kuyaendesha maisha yake.Nilifika hadi mahala alikokuwa akiishi na wenzake.kwa kweli wanaishi maisha mabaya sana.Mwanzoni  Marina alikuwa mgumu kukubali kubadilisha aina ya maisha anayoyaishi.Alikwisha kata tamaa na maisha yake.Siku ya pili tangu nimemfahamu nilipigiwa simu na mjumbe wa eneo analoishi Marina kwamba Marina pamoja na wenzake wawili wamekamatwa kwa wizi wa simu ,nilikwenda kumtoa polisi na kulipa vifaa vyote ambavyo yeye na wenzake walikuwa wakituhumiwa kuviiba.Matatizo yalianza baada ya kutoka polisi kwani alianza kuumwa sana ikanibidi kumpeleka hospitali akapata matibabu halafu nikampeleka nyumbani kwetu.Kule nyumbani kwetu mambo hayakuwa mazuri sana ,wazazi hawakupendezwa na kitendo cha mimi kumpeleka Marina akaishi pale.Siku iliyofuata nikiwa kazini nilipigiwa simu kwamba Marina ameondoka nyumbani.Nikaenda tena kumtafuta na kumkuta kule alikokuwa akiishi na wasichana wenzake.Nilimchukua na kumpeleka tena hospitali kwani hakuwa akijisikia vizuri.Baada ya uchunguzi ikagundulika kwamba ana matatizo ya figo kwa hiyo inabidi abadilishiwe figo nyingine.Jana jioni nilirudi naye tena nyumbani lakini ukatokea mtafaruku baina yangu na mama ambaye hakuwa akitaka Marina akae pale nyumbani.Niliumia sana kwa kitendo kile na hivyo ikanilazimu kuondoka nyumbani na kwenda kuchukua chumba katika hoteli.Usiku wa manane hali ya Marina ilibadilika ikanibidi nimkimbize hospitali ambako bado amelazwa hadi sasa.Kwa maana hiyo Marina ni mtu asiye na ndugu wala mtu wa karibu ambaye anaweza akamshughulikia au kuyajali matatizo yake.kwa sasa mtu pekee ambaye anaweza kumuita ndugu ni mimi . Marina anahitaji msaada mkubwa na wa haraka.Kama kuna lolote unaloweza kufanya ili kuaokoa maisha yake tafadhali naomba unisaidie” Innocent akasema.



0 comments:

Post a Comment

Followers

 

BONYEZA "LIKE" NA UJIUNGE NASI MOJA KWA MOJA KWA SIMULIZI MPYA KILA SIKU

Powered By masimulizi