Saturday, April 26, 2014

SERENA SEHEMU YA 22









            “Jana mchana limetokea tena tukio jingine.Mtoto wa kwanza wa mzee Albano aitwaye Serena gari lake lilishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana na kusababisha kifo cha mtu mmoja.Mtu huyo,kijana mwenye umri wa miaka 23 ambaye amejulikana kuwa ni mkaazi wa Kiwalani ,aitwaye Salum Ahmed alikuwa ni mfanyakazi wa Papaya group na aliambiwa na bosi wake aipeleke ile gari Rosela restaurant ambako binti huyo wa mzee Albano alikuwa akipata chakula akiwa na Dr Jason.Kwa mujibu wa mashuhuda gari lile lilipofika katika geti la kuingilia hapo hotelini ikatokea pikipiki iliyobeba watu wawili na kijana aliyekuwa amepanda nyuma akaanza kuimiminia risasi gari ile ya Serena na kusababisha kifo cha yule kijana aliyekuwa katika ile gari .Asubuhi ya siku ya leo tumepokea taarifa toka hospitalini hapo kuwa mzee Albano haonekani hospitalini.Ametoweka katika mazingira yenye utata sana kwani mzee huyu hana fahamu na kama ametoweka basi lazima kuna mtu au watu waliotoa hapo hospitali.Tumeongeza askari ili kuimarisha ulinzi katika eneo zima la hospitali Mpaka sasa hivi tunavyoongea bado upekuzi unaendelea lakini hakuna dalili zozote za kumpata mzee Albano.Hii inatufanya tuamini kwamba mzee yule ametoroshwa na watu wenye nia mbaya ambao wamekuwa wakijaribu kumuua bila mafanikio.Kutokana na mlolongo huu wa matukio ambayo yote yanahusiana na mzee Albano pamoja  na familia yake moja kwa moja tumeona kuna kila ulazima wa kuunda kikosi kazi kidogo ambacho kitalishughulikia suala hili kwa haraka sana na mwisho wa siku kuhakikisha mzee Albano anapatikana na kuwabaini watu hawa waliofanya kitendo hiki kiovu na kuhatarisha uhai wa mzee huyu .Tunachotakiwa kukifanya kwanza ni kujua mahali alipo mzee Albano na kumuokoa kabla ya watekaji hawa hawajakeleza mpango wao ambao ninaimani wana lengo la kumuua kwa sababu toka mwanzo walikwisha onesha dalili mbaya.Pili ni kupata ukweli wa nini sababu ya wao kumteka mzee Albano.Nini sababu ya kutaka kumuua.Tatu nini sababu ya kutaka kumuua binti wa mzee Albano na hapo hapo  mchunguze kama shambulio lile la gari la Serena lina uhusiano wa moja kwa moja na mzee Albano.Nne wote waliohusika katika mpango wote huu watiwe nguvuni haraka iwezekanavyo”         Kamanda Barnabas akatoa maelekezo kwa kikosi kazi hiki alichokiteua halafu akawaamuru waanze kazi mara moja na wahakikishe wanampata mzee Albano akiwa hai ndani ya kipindi kifupi


0 comments:

Post a Comment

Followers

 

BONYEZA "LIKE" NA UJIUNGE NASI MOJA KWA MOJA KWA SIMULIZI MPYA KILA SIKU

Powered By masimulizi