Wednesday, April 9, 2014

BEFORE I DIE SEHEMU YA 8







            “Mzee Mustapha ukweli ni kwamba mimi sikuwa nimewafuata makahaba.Mimi ni kijana niliyelelewa katika maadili mazuri,familia yetu inauwezo mkubwa kiuchumi na hata kiwanda hiki ni mali ya familia.Katika maisha yangu sikuwahi kuota kama iko siku ningeweza kuwafuata wasichana kama wale.Kwa ufupi tu nikwamba mimi huwa ninaumia sana moyo ninapomuona binadamu mwingine akiteseka ama kuishi maisha ya shida hali mimi nina uwezo wa kutosha.Nimekuwa nikisaidia watu wengi tu ili waweze kuondokana na maisha wanayoyaishi .Siku ya jumamosi nikiwa na dada yangu na rafiki zetu kadhaa tulikwenda katika klabu moja ya burudani ili kustarehe kidogo baada ya shughuli za wiki nzima.Tukiwa pale nilimuona msichana ambaye baadae nilimtambua kama Marina akiwa kati kati ya kundi la makahaba.Kwa kweli niliumia sana na kujiuliza ni kitu gani kilipelekea msichana mdogo kama yule kuwapo usiku ule na makundi kama yale.Nilikuwa na nia ya dhati ya kumsaidia ,lakini kwanza nilitaka kumfahamu japo kwa undani kidogo ili nione ni jinsi gani nigeweza kumsaidia.Nilifanikiwa kuondoka naye kama mtu niliyekuwa nikitaka kulala naye kwa usiku.Nilikwenda naye hotelini lakini si kwa lengo la kufanya naye mapenzi kama yeye alivyokuwa akifikiri..Nilichokuwa nakitaka ilikuwa kumfahamu japo kwa ufupi na kujua sababu zilizopelekea yeye kujiingiza katika biashara ile .Alinieleza historia yake kwa ufupi ambayo kwa kweli inasikitisha sana.Nilimuonea huruma na kuamua kwa moyo wa dhati kabisa kumsaidia.Marina hakuwa tayari kwa msaaada niliokuwa nataka kumpatia ikiwa ni pamoja na kumpeleka shule na baadae kumtafutia kazi nzuri na kuyabadili maisha yake.Sikukata tamaa nikaamua kwenda naye hadi mahala anapoishi ili nione ni maisha ya namna gani anayaishi.Nilistuka sana na aina ya maisha wanayoishi wasichana wale baada ya kufika mahala anapoishi Marina.Nilishindwa kukaa katika chumba chao nikatoka nje.Pale nje nikafuatwa na mwanamke mmoja ambaye alionekana kama ndiye mkubwa wao akaniomba niingie ndani.Nilikubali nikaingia ndani na ndipo hapo purukushani ilioanza Walidai eti ni lazima nifanye mapenzi nao wote.Sikuwa tayari kwa upuuzi ule ndipo hapo vurugu ilipozuka hadi pale ulipotokea na kuniokoa toka mikononi mwa makahaba wale.Kibaya zaidi ni kwamba wakati nataka kufanyiwa mambo yale ya ajabu Marina alikuwa akiniangalia huku akivuta sigara yake akitabasamu.Inaonekana alikuwa amefurahi mimi kufanyiwa vile.Wema wangu,fadhila zangu vyote hakuviona kabisa.Nasikitika sana Mzee Mustapha kwa mambo waliyonifanyia,lakini mimi sikuwa nimekwenda pale kwa ajili ya kutafuta mapenzi,bali nilikuwa na lengo zuri la kutaka kumsaidia Marina.” akasema na kukaa kimya kwa muda huku akimtazama Mzee Mustapha.




0 comments:

Post a Comment

Followers

 

BONYEZA "LIKE" NA UJIUNGE NASI MOJA KWA MOJA KWA SIMULIZI MPYA KILA SIKU

Powered By masimulizi